Logo

‘Bendera nyekundu’ za kuepuaka ndani ya mapenzi – Maisha Magic Bongo

Habari
24 Februari 2023
Orodha ya baadhi ya vitu kuepuka ndani ya mahusiano mwezi huu wa mapenzi
Article

1677312625 27 untitled design  3

Kuna baadhi ya mahusiano ndani ya vipindi vya Maisha Magic Bongo ambayo yanatuacha tukijiuliza kwanini bado hao wanandoa bado wapo pamoja? Soma hapo chini kujua ni vitu gani vya kuviepuka ndani ya mapenzi

Kuachana kila mara (Regina na Edu)
Ingawa Edu na Regina wana mtoto pamoja na wanadai kupendana, mahusiano yao wamekuwa hayaeleweki na kila mara wanachana na kurudiana. 

1677503054 28 screenshot 2023 02 24 at 14.30.56

Kutoaminiana (Doris na Roy – Huba)
Baada ya Roy kutofanyikiwa kuchagua kati ya Nandy na Doris, aliamua kuwaoa wote wawili. Kwa sasa hivi, baada ya Nandy kurudi mjini Roy azidi kuficha mahusiano yake na Nandy kwa Doris wakati pia akimficha Nandy kuhusu mahusiano yake na Doris.

1677503213 28 screenshot 2023 02 21 at 19.25.51

Uongo (Maria na Frank)
Ingawa Maria alivishwa pete na Frank, bado anamahusiano ya kichini na Thomas. Sasa itakuaje baada ya kuamua kufunga ndoa wakiwa bado na uongo ndani ya mahusiano yao.

1677503365 28 jua kali

Usikose kuangalia tamthilia zote uzipendazo ndani ya DStv chaneli 160! Jibu swali hilo hapo chini 👇