Vivian na Sidi wamekuwa wakificha mahusiano yao kwa familia zao na marafiki zao. Sidi alijikuta ameingia ndani ya mahusiano na JB mume wa mwanae wa kambo, Tima. Mahusiano ya JB na Sidi yalianza baada ya Kashaulo kuhama toka nyumbanikwa JB, Sidi alijikuta akianza kusikia hisia kwa JB na walianza mahusiano ya kisiri. Kwa sasa Sidi anataka kuachana na Jb.
Sidi ndani ya Huba
Vivian na Michael walianza na mapenzi yao ya siri baada ya Michael kuachwa na mke wake baada ya mke wake kubeba mimba ya Frank. Kwa sasa Michael alimuomba Vivian amuoe lakini adai kwamba wazidi kuweka penzi lao siri kwa sasa hivi.
Vivian ndani ya Jua Kali
Kumbuka kufuatilia kipindi cha Huba kila Jumatatu hadi Ijumaa saa 3 usiku na pia Jua Kali kila Jumatano hadi Jumapili saa 3:30 usiku ndani ya #MaishaMagicBongo pekee!