Baada ya muda wa kuwa kati ya Nandy na Doris, hatimaye Roy aameamua kuwaoa wote wawili. Mpango wa Roy ulikuwa aachane na Doris kabisa ili awe na Nandy. Tatizo lilikuja kabla yakumuacha Doris, Roy aligundua kwamba Doris ni mjauzito.
Kwasababu Roy hakulelewa na baba yake, hakuona ni sawa kumuacha Doris wakati akiwa ni mjamzito. Aliaamua kubaki naye, ili wamlee mtoto Pamoja. Lakini Roy hampendi Doris na hataki kuwa nae, bado anampenda Nandy.
Baada ya kujadili, Doris na Roy walikubaliana kwamba ni lazima awaoe wote wawili. Doris aling’ang’ania kuwa mke wa kwanza. Tatizo likaja baada ya Bi Sikitu, mama yake Doris, kuona nyota zilizo mwambia kwamba ni lazima Nandy awe mke wa kwanza. Doris alikasirika na kuamua kufanya harusi yake siku ya karibu zaidi na hili jambo lili mlazimisha Nandy kuamisha harusi yake pia.
Kati ya hizi harusi mbili, ungepata mwaliko ungehudhuria harusi gani? Piga kura yako hapo chini.
Pia kumbuka kuangalia #MMBHuba kila Jumatatu hadi Ijumaa saa 3 usiku ndani ya chaneli 160!
