Logo
Jiya
channel logo dark

Jiya

160DramaPG13

Jinsi ya Kujiponya Baada ya Kupata Mvunjiko wa Mahusiano - Jiya

Habari
18 Aprili 2024
Jiya avunja mahusiano na Don G na pia akataa kuolewa na Sanjeet ndani ya siku moja. Je kati ya hawa wawili wewe nini nani ukiachika?
Jiya

Kuvunjika kwa mahusiano kunaweza kuwa kama tetemeko la ardhi moyoni mwako. Hamna anayejui maumivu haya zaidi ya Jiya, baada na kuachanana watu wawili. Lakini, kama vile ardhi inavyojirekebisha baada ya tetemeko, hivyo ndivyo moyo wako unaweza kupona kutokana na maumivu ya mapenzi.

Angalia: Jiya alivyomuacha Sanjeet kwenye siku yao ya ndoa

Hapa kuna hatua tano muhimu za kujiponya baada ya kuvunjika kwa mahusiano:

  1. Kukubali na Kupokea Hisia Zako

 Ni muhimu kukubali hisia zako kikamilifu. Usijaribu kuzima au kuficha hisia hizo. Kulia au kusikia uchungu ni sehemu ya mchakato wa kupona. Kujipa ruhusa ya kuhisi hisia zote kunaweza kusaidia kuzipunguza hatua kwa hatua.

  1. Tambua Sababu za Kuvunjika

 Kujiuliza maswali magumu kuhusu sababu za kuvunjika kwa mahusiano kunaweza kusaidia katika mchakato wa kujiponya. Jitahidi kuelewa ni nini kilichochangia kuvunjika kwa uhusiano na jinsi unavyoweza kujifunza kutokana na hilo ili kuboresha maisha yako ya baadaye.

  1. Tenga Muda wa Kujitunza

 Baada ya kuvunjika kwa mahusiano, ni muhimu kujitunza kwa upendo na kujali. Jitahidi kufanya mambo ambayo hukufurahia na kujipa muda wa kujielewa upya bila kuwa na presha ya mahusiano mapya. Jitahidi kujenga upya uhusiano mzuri na wewe mwenyewe.

  1. Kuwa na Msaada wa Kihisia

Hakikisha una watu wa karibu ambao unaweza kuzungumza nao na ambao wanaweza kukusaidia kupitia kipindi hiki kigumu. Marafiki, familia au hata mshauri wa kihisia wanaweza kutoa msaada na faraja ambayo unahitaji.

  1. Jenga Mipango ya Baadaye

Ingawa inaweza kuwa ngumu kufikiria mbele wakati unapopitia maumivu ya sasa, ni muhimu kuanza kuweka malengo na mipango ya maisha yako ya baadaye. Fikiria juu ya mambo unayotaka kufikia na jinsi unavyoweza kufikia malengo hayo peke yako au pamoja na watu

Angalia: Don G alivyokasirika baada ya kuachwa na Jiya

Kumbuka kufuatilia kipindi cha #MMBJiya kila Jumatatu hadi Jumatano saa 1:30 usiku ndani ya DStv chaneli 160, na marudio kila Jumapili saa 10 mchana.