Kipindi hiki kinazungukia kundi la watu watatu, Angel, Pipi na Mo. Pamoja wanafanya biashara ya kuwatapeli watu jijini Dar es Salaam. Pata kujua Zaidi nani ni nani ndani ya tamthilia hii.
Angel
Angel ndio mwongozaji wa kundi hili la Danga. Angel ndio akili nyuma ya kila kiyu wanachofanya. Aliingia kwenye haya Maisha baada ya mume wake kufariki, ingawa Maisha haya yamesha muweka baba yake kwenye hatari bado anaendelea.
Pipi
Pipi ndiye mrembo wa kundi hili, kazi yake Pipi ni kuwa karibu na watua ambao wanawaibia. Ukaribu waku unaweza kufikia ata mapenzi, mpaka wamuamini.
Mo
Mo ndiye nguvu ya kila kitu. Kama mwanaume pekee kazi ya Mo ni kuwalinda Angel na Pipi kwenye kazi zao.
Inspector Mwana
Ni polisi amabaye ana hamu ya kuwakamata wakina Angel, lakini kwa bahati mbaya hana Ushahidi wa kutosha wa kuwakamata.
Don
Kibosile mwenye pesa nyingi, wakina Angel wana mperereza ili wamuibie.
Lucy
Mfanya kazi mpya nyumbani kwa Don. Anadai kwamba hana pa kwenda na hana pesa, ni mama wa mtoto mmoja na mama yake ndio katoka jela. Aliomba kuja kufanya kazi kwa Mzee Don na mke wake, je inawezekana kwamba alitumwa na Angel kumperereza Don?
Usikose kipindi cha #MMBDanga kila Jumatatu hadi Jumatano saa 1:30!