Siri kubwa zilitobolewa ndani ya kipindi cha Jua Kali mwaka huu. Soma orodha hiyo hapo chini kusoma siri kubwa zilizo funununika mwaka huu.
Mama Michael
Baada ya Michael kugundua kwamba mke wake alizaa na Frank na mtoto ambaye alikuwa akifikiria ni wa kwake sio wake. Hili jambo limvunja moyo Michael kwasababu alikuwa na hamu ya mtoto. Baada ya hapo mama yake aliamua kumuweka wazi kwamba anamtoto wakiume aliyezaliwa kipindi alivyokuwa mwanafunzi na baada ya kufanya vipimo.
Prof Bill
Baada ya kuishi na mfanyakazi wao Zai kwa miaka tangu alivyomuoa mke wake, siri kubwa ilifichuka kwa Profesa kwamba yeye ndiye aliyekuwa mtoto wa Zain a aliamua kumfanya Zai awe mke mwenza na Mrs Bill.
Femi
Badala ya muda ya Femi na Lukas kukosana juu ya Lukas kufikiria kwamba Femi alikuwa anatembea mwanaume mwingine. Hatimaye Femi aliamua kuwa mkweli na Lukas na kumwambia kama ana kansa yad amu.
Maria
Mwanakondoo Maria amekwa baada ya kugundua kama anaujauzito na ujauzito ni wa Thomas ingawa anamahusiano na Frank. Maria anampango wa kumsingia Frank hii mimba kwa sababu mahusiano yake na Thomas bado ni siri.
Eva
Kwa muda mrefu Eva amekuwa akimkwepa Bill Jnr baada ya Bill kumwambia kwamba anampenda. Hatimaye aliamua kumwambia Bill ukweli kwamba kabla ya kuwa kijakazi aliwahi kuwa changudoa mtaani na ajua hali yake ya kiafya.
Stella
Baada ya kujaribu kurudiana na mume wake Thomas wakati akiendelea mahusiano kijana wa Thomas, Felix, Thomas aligundua ukweli na aliamua kumpa talaka Stella,
Usikose kipindi cha #MMBJuaKali kila Jumatano hadi Jumamosi saa 3:30 usiku ndani ya #MaishaMagicBongo.