AGAINST CRIME
12:20 EAT
7 APRILI 2016

Leo, tunamkumbuka muigizaji mashuhuri, SuperStar wa filamu za Bongo, rafiki, ndugu, mwana wa Tanzania, Marehemu Steven Kanumba.
Kazi yake ya uigizaji na uzalishaji wa filamu za Bongo zilileta upya wa maudhui na burudani. Alitufungulia njia katika biashara ya burudani katika Afrika na ulimwengu kwa jumla. Ndugu Kanumba, lala salama, Mwenyezi Mungu amweke mema.
Katika filamu ya leo,Fur anafuatwa na maovu ya wazazi wake waliofanya biashara ya kuuza madawa ya kulevya. Mamake Mzazi aliuwawa na mhalifu aiitwaye Moko, isitoshe, mchumba wake ametekwa nyara! Roho ya Fur imejaa chuki na uchungu wa mwana aliyeaachwa na mama.
Ungana nasi kupata kisa hiki tukimkumbuka Mwigizaji mashuhuri, SuperStar wa filamu za Bongo, Marehemu Steven Kanumba!
Wasiliana nasi katika kurasa zetu za facebook, Twitter na WeChat.