Logo
Nuru
channel logo dark

Nuru

160DramaPG13

Mwangaza Waendelea: Msimu wa Pili wa Nuru Kutua Mei 20!

Habari
16 Mei 2024
Msimu wa pili wa Nuru kuanza Mei 20 saa 4 usiku ndani ya Maisha Magic Bongo
Nuru

Watazamaji wetu wapendwa wamekuwa wakiuliza kwa muda mrefu lini msimu wa pili wa #MMBNuru utaanza tena hatimaye subira inaisha. tamthilia ya Nuru inahusu ndugu wawili waliochukiana wanajikuta lazima waungane kupambana na adui anaewatandia giza nene maishani mwao, baba yao. Hapo chini ni matukio wakubwa yaliyotokea ndani ya msimu wa kwanza:

Mahusiano ya Ritha na Ronald

Baada ya kugundua kwamba Ritha alikuwa akicheat na Adrian, Ronald alianza mahusiano yake pembeni lakini aliamua kumsamehe Ritha. Baada ya Naomi kumkuta John na Alice, pacha wake wa kufanana na Ritha, alimwambia Adrian. Sasa Adrian alibaki kudhani kwamba Ritha alirudia kumcheat, Ronald aliamua kufanya maisha kivyake wakati muda wote mtu aliyedhani ni Ritha alikuwa pacha wake Alice.

Adrian na Naomi

Baada ya kushindwa kupata kampuni ya Mzee Andrew, Adriam aliamaua kujaribu kumtongoza Naomi.

Mzee Andrew na Juliana

Baada ya Jualiana kukutana na Mzee Andrew aliacha na mama yake aliyekuwa kimtesa na alihamia kwa Mzee Andrew lakini anasiri kubwa ya Adrian.

Alice agundua kwamba ana pacha

Baada ya Ritha kumgundua Alice na kumleta ofisini, Alice agundua kwamba Ritha anaweza kuwa pacha wake aliyepotea zamani.

Danny na mke wake

Baada ya kukataliwa na Jualiana Danny aliamua kufanya bidi nyumbani lakini mke wake amekuwa akimroga.

Ronald na Doreen

Baada ya Ronald kuanza mahusiano na Doreen, watazamaji waligundua kwamba Doreen amekuwa akimtapeli Ronald na msimu uliopita alidai kwamba ana ujauzito.

Ni nani unahamu zaidi ya kumuona ndani ya msimu wa pili wa #MMBNuru.

Msimu wa pili wa Nuru

Je ni nani unahamu ya kuonana nae tena?

Nuru
Mahusiano ya Ritha na Ronald0%
Nuru
Adrian na Naomi0%
Nuru
Mzee Andrew na Juliana2%
Nuru
Alice na Ritha2%
Nuru
Danny na mke wake1%
Nuru
Ronald na Doreen94%

Usikose vipindi vipya kila Jumatatu hadi Ijumaa saa 4 usiku ndani ya MaishaMagicBongo.

Pata kujua waigizaji wa tamthilia hii hapa: