Ni Malkia wa nguvu, Mrembo, shupavu na mwenye kipaji cha pekee Yvonne Cherrie anayejulikana kama @monalisatz ni miongoni wa wasanii wa filamu wakongwe nchini waliofanikiwa kuiweka bendera ya Tanzania sehemu nyingi duniani.Kupitia kipindi chetu cha Maishayangu alisema mengi aliopitia hadi kapata kuwa msanii maarufu
Yvonne Cherrie alizaliwa tarehe 19 , Agosti 1981. Ambaye ni mama wa mtoto moja anasema kufanikiwa kwake na kipaji chake kilionekana akiwa na umri mdogo sana na huenda ikachagiwa na mama yake Mzazi ambaye pia ni mmoja wa wasanii wakongwe Tanzania.
Mafanikio yake yanamuweka kileleni na kumpeleka sehemu mbali mbali duniani , nchi nyingi za Africa na barani ulaya na amejipatia tuzo mbbalimbali nje na ndani ya nchi.
Kwa sasa Monalisa anjihusisha na uandaji na uongozaji filamu, anajihusisha na maswala ya ubalozi wa mambo ya Sanaa na pia ana bishara ya vitu vya asili.
Ili kuona stori zingine nyingine kama hizi za kusisimua, tazama Maisha Yangu kila Jumanne saa 3:30 usiku ndani ya DStv 160 pekee!
