Logo
MMB HubaSM V1 TwitterCover Generic HR
channel logo dark

Huba

160Tamthilia16

Vipindi halisi vya Tanzania unovyoweza kufurahia siku ya Uhuru

Habari
08 Decemba 2021
Maisha Magic Bongo iko pamoja nawe siku kuu hii ya Uhuru.
Porcelain Dinnerware eBay Billboard

Wakati tunaazimisha siku hii ya miaka 60 ya uhuru, tunapenda kuwakumbusha vipindi bomba vya Kitanzania ndani ya Chaneli 160. Kianziazia asubuhi mpaka usiku unaweza kupumzika na kupata burudani za kipekee ndani ya Maisha Magic Bongo:

Danga saa 6 mchana (marudio)

Anza siku yako ukiburudika na kipindi cha Danga, marudio ya kipindi cha jana yatacheza saa 6 mchana. Hiki kipindi kinachohusu madada wawili, Angel na Pipi pamoja na rafiki yao wa kiume, Mo. Pamoja wanafanya kazi ya wakuwadhulumu matajiri chini Tanzania wakitumia urembo wao, akili na miunganisho yao. Kwa vipindi vipya usikose kuangalia kila Jumatatu hadi Ijumaa saa 1:30 usiku.

Bass saa 11 jioni

Pata kipindi kipya cha Bass ambacho kitakuletea burudiani kwa njia ya muziki. Burudika na miziki ya kisasa ambayo inavuma sana kwenye chati. Pia unaweza kuangalia mahojiano na mastaa wa Bongo Flava wanaovuma nchini.

Harusi Yetu saa 1 usiku

Jiunge na mtangazaji wetu mpya, Precious Myner kwenye kipindi kipya cha #MMBHarusiYetu ambacho kitakuwa kinaonyesha harusi ya wiki hii. Burudika na harusi ya halisia ya kitazania kuanzia stori ya njisi walivyo kutana, angalia kitchen party, send off, harusi yenyewe mpaka ukumbini.

Huba saa 3 usiku

Huba ni kipindi kipenzi sana nchini Tanzania, kipindi hiki kina husu mapenzi na jinsi watu wanavyoweza kufanya ubaya na pia uzuri  kutokana na huba. Jiunge nasi leo usiku kuangalia kama mahusiano kati ya Devi na Nelly yataendelea? Na je Tima atamuacha Jude?

Jua Kali saa 3:30 usiku

Kipindi cha Jua Kali kinahusu Professa Bill, ambaye pamoja na Thomas wanaendesha kampuni ambayo wanatumia kudhulumu watu. Wakati pia kukiwa na shida tofauti ndani ya familia za Bill na Thomas.

La Familia saa 4 usiku

Tamthilia hii inazungukia familia ya Bibi na Bwana Ibrahim, familia yao yenye watoto watano. Baada ya Bwana Ibrahim kumteua mtoto wake wa kwanza wakiume, Raphael, kuwa mkuu wa kampuni ya familia, binti yake wa kwanza Violeth akasirika na kuanza vita na familia.

Ni kipindi gani utaangalia leo?

Ni kipindi gani cha Kitanzania utaburudika nacho leo? tuambie hapo chini ??

Bass1%
Harusi Yetu14%
Huba36%
Jua Kali38%
La Familia11%

Tunakutakia siku njema ya uhuru, na tunakushukuru kuendelea kuchagua Chaneli ya Maisha Magic Bongo!