Migongano na Changamoto za kifamilia
Ingia ndani kabisa ya maisha ya familia ya Diwani na Shakombo. Shuhudia mapambano ya madaraka, vifungo vya urafiki, na uzito wa urithi huku familia mbili zikiingiliana katika safari ya upendo, siri, na uaminifu.
Hadithi ya Mapenzi yenye Siri
Kiini cha Chanda ni mapenzi kati ya Yaz na Azra. Kutoka kwa harusi ya kifahari ya Uswahilini hadi changamoto wanazokabiliana nazo, safari yao imejaa shauku, siri, na uaminifu usioyumba.
Wahusika wakike wenye nguvu
Pata uzoefu wa nguvu na uthabiti wa wahusika kama Dida Diwani, ambaye anawajibika katika jukumu lake kwa uthabiti, matamanio, na mguso wa hila, na Azra, ambaye anaonyesha uthabiti na uaminifu anapokabiliwa na dhiki.
Mafumbo na mafunuo
Kwa ukweli uliofichwa, mahusiano ya zamani, na siri za familia, Chanda anaahidi hali ya hisia na misukosuko isiyotarajiwa kila kukicha.
Kuzamishwa kwa tamaduni
Kipindi hiki kinatoa mchanganyiko wa kipekee wa mila, usasa, na utata wa matarajio ya jamii.
Waigizaji nyota
Tamthilia hii imeshirikisha baadhi ya waigizaji mashuhuri wa Tanzania kama vile Feza Kessy, Mwijaku, Christopher Mziwanda, Hidaya Njaidi na Mayasa Mrisho, Chanda amewaweka waigizaji wake kama wasanii bora zaidi nchini, na kuhakikisha mikasa ya nguvu inayo wavutia watazamaji.
Ronald Shelukindo, Mkuu wa Masoko wa MultiChoice Tanzania, anasema, "Tunaamini Chanda itaunda mazungumzo na mijadala ambayo itasikika kwa watazamaji. Kipindi hiki kinadhihirisha dhamira yetu ya kutoa burudani ya hali ya juu. Iwapo hujafanya hivyo, tunakuhimiza ujiunge na DStv na uwe sehemu ya safari hii ya kasi ya kusisimua."
Picha: Ronald Shelukindo (Mkuu wa Masoko wa MultiChoice Tanzania)
Wakati pazia la uhondo huu litafunguliwa Jumatatu, Oktoba 2 saa 1:30 usiku, jiandae kufurahishwa na Chanda kwenye Maisha Magic Bongo, DStv Channel 160 kila Jumatatu hadi Jumatano.
Kwa zaidi: